Mourinho:Chelsea mambo shwari sasa
Matokeo yamemridhisha meneja Jose
Golkipa wa Chelsea, Petr Cech, aliokoa mabao kadhaa katika kipindi cha pili cha mechi kati ya Chelsea na Crystal Palace na kusalia na pointi mbili tu kufikia Arsenal wanaoongoza orodha kwa pointi.
Fernando Torres aliiweka Blues mbele katika uwanja wa Stamford Bridge baada ya shuti la Willian kugonga lango la bao na kuwakosesha bao lengine.
Mlinda lango, Cech aliwakosesha mabao Jason Puncheon, Damien Delaney na hatimaye Stuart O'Keefe huku wenyeji wakishinda kwa leo.Crystal Palace hata hivyo walisawazisha kupitia kwa mchezaji, Marouane Chamakh kabla ya Ramires kuiweka Chelsea kifua mbele kwa mabao mawili kwa moja.
Wenyeji walifanikiwa kushinda kutokana na mabao yao ya dakika za mwisho 2-1.
Meneja wa klabu Jose Mourinho alisema kuwa Chelsea walikuwa matatani hasa baada ya kushindwa na Stoke wikendi iliyopita. Lakini sasa mambo shwari.
No comments:
Post a Comment