Mkalimani huyo Thamsanqa Dyantyi alionekana jukwaani na kutafsiri kwa alama hotuba zilizotolewa na viongozi mbambali katika uwanja wa FNB mjini Soweto ambao ulitumika kwa kumbukumbu hiyo siku ya jumanne.
Mapema leo alhamisi Bwana Dyantyi amejitokeza mbele ya vyombo vya habari na kuomba radhi kwa madai kuwa alikuwa na matatizo ya kiafya yaliyoathiri utendaji kazi wake.
Wanachama wa jamii ya watu wenye ulemavu wa kusikia na kuongea nchini Afrika Kusini walilalamikia kitendo hicho na kutaka serikali ichukue hatua kali.
Lakini Chama tawala cha ANC kimesema kimekuwa kikimtumia Mkalimani huyo mara kadhaa katika shughuli zake na hajawahi kulalamikiwa kuwa na matatizo ya kiafya wala ubora wa kazi yake.
Taasisi inayotoa elimu ya Kutafsiri lugha za alama ilisema tayari iliishawasilisha malalamiko dhidi ya Bwana Dyantity, lakini ANC haikuchukua hatua zozote.
Mapema leo alhamisi Bwana Dyantyi amejitokeza mbele ya vyombo vya habari na kuomba radhi kwa madai kuwa alikuwa na matatizo ya kiafya yaliyoathiri utendaji kazi wake.
Wanachama wa jamii ya watu wenye ulemavu wa kusikia na kuongea nchini Afrika Kusini walilalamikia kitendo hicho na kutaka serikali ichukue hatua kali.
Lakini Chama tawala cha ANC kimesema kimekuwa kikimtumia Mkalimani huyo mara kadhaa katika shughuli zake na hajawahi kulalamikiwa kuwa na matatizo ya kiafya wala ubora wa kazi yake.
Taasisi inayotoa elimu ya Kutafsiri lugha za alama ilisema tayari iliishawasilisha malalamiko dhidi ya Bwana Dyantity, lakini ANC haikuchukua hatua zozote.
No comments:
Post a Comment