Akizungumza katika mahojiano na kituo kimoja cha televisheni leo jumatatu, Yingluck amesema uchaguzi pekee ndio utakuwa njia sahihi kwa watu wa Thailand kuamua kile wanachokitaka.
Baada ya ghasia na maandamano kwa takribani mwezi mmoja Yingluck amesema uchaguzi huo ukafanyika mwishoni mwa mwezi January au February mwaka ujao.
Waziri Yingluck amesema watu wengi wa makundi mbalimbali wanapinga serikali na njia bora ni kuwapa nafasi watu wa Thailand kuamua kupitia uchaguzi.
Hata hivyo waandamanaji wameapa kuendelea na maandamano kwa madai kwamba serikali ya Yingluck inaongozwa na kaka yake Thaksin Shinawatra, ambaye anaishi uhamishoni baada ya aliondolewa mamlakani.
Kiongozi wa maandamano hayo, Suthep Thaugsuban amesema hatasitisha maandamano hayo mpaka azma yao itakapokamilika.
Baada ya ghasia na maandamano kwa takribani mwezi mmoja Yingluck amesema uchaguzi huo ukafanyika mwishoni mwa mwezi January au February mwaka ujao.
Waziri Yingluck amesema watu wengi wa makundi mbalimbali wanapinga serikali na njia bora ni kuwapa nafasi watu wa Thailand kuamua kupitia uchaguzi.
Hata hivyo waandamanaji wameapa kuendelea na maandamano kwa madai kwamba serikali ya Yingluck inaongozwa na kaka yake Thaksin Shinawatra, ambaye anaishi uhamishoni baada ya aliondolewa mamlakani.
Kiongozi wa maandamano hayo, Suthep Thaugsuban amesema hatasitisha maandamano hayo mpaka azma yao itakapokamilika.
No comments:
Post a Comment