Bado kumekuwapo na misafara na misururu mirefu kuelekea kwenye ikulu ya nchi hiyo mjini Pretoria, ambapo mwili wa kiongozi huyo unalala hapo kwa siku tatu.
Wakati wananchi wa Afrika kusini wakiendelea kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Nelson Mandela mjini Pretoria, raia wa kigeni nao wameendelea kufurika nchini humu kutoa heshima zao kwa mwili wa Mandela huku wakimlilia wakisema aliwaunganisha na kuwapa hata uraia licha ya kuwa walitoka nje ya Afrika Kusini.
Familia ya Mandela imesema imeguswa na jinsi umati wa watu waliofika kutoa heshima ya mwisho kwa mpendwa wao, na hiyo ni ishara ya kuthamini matendo mema ambayo yalifanywa na Hayati Mandela.
Mamia kwa maelfu ya watu maarufu duniani wakiwemo Wakuu wa nchi mbalimbali walihudhuria ibada maalumu ya kumkumbuka Mandela siku ya jumanne, Rais wa Marekani Barack Obama ni miongoni mwa viongozi wa Kimataifa waliohudhuria kumbukumbu hiyo.
Mwili wa Mandela unatarajiwa kuzikwa siku ya jumapili ya tarehe 15 mwishoni mwa juma katika kijiji cha Qunu.
Wakati wananchi wa Afrika kusini wakiendelea kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Nelson Mandela mjini Pretoria, raia wa kigeni nao wameendelea kufurika nchini humu kutoa heshima zao kwa mwili wa Mandela huku wakimlilia wakisema aliwaunganisha na kuwapa hata uraia licha ya kuwa walitoka nje ya Afrika Kusini.
Familia ya Mandela imesema imeguswa na jinsi umati wa watu waliofika kutoa heshima ya mwisho kwa mpendwa wao, na hiyo ni ishara ya kuthamini matendo mema ambayo yalifanywa na Hayati Mandela.
Mamia kwa maelfu ya watu maarufu duniani wakiwemo Wakuu wa nchi mbalimbali walihudhuria ibada maalumu ya kumkumbuka Mandela siku ya jumanne, Rais wa Marekani Barack Obama ni miongoni mwa viongozi wa Kimataifa waliohudhuria kumbukumbu hiyo.
Mwili wa Mandela unatarajiwa kuzikwa siku ya jumapili ya tarehe 15 mwishoni mwa juma katika kijiji cha Qunu.
No comments:
Post a Comment