ABIRIA WALIOKUWA WAKISAFIRI NA BASI LA UKINGA EXPRESS WANUSURIKA KIFO KUFUATIA AJALI MBAYA WILAYANI MAKETE
Abiria waliokuwa wakisafiri kwa basi la Ukinga Express kutoka Njombe kwenda Makete mkoani Njombe, wamenusurika kifo baada ya basi hilo walilokuwa wakisafiria kuigonga fuso kwa nyuma iliyokuwa imepata hitilafu na kuegeshwa barabarani
Ajali hiyo imetokea usiku wa kuamkia leo katika eneo linalohofiwa na wengi la Lwamadovela kata ya Tandala wilayani Makete, baada ya dereva wa basi hilo kuigonga kwa nyuma fuso hiyo ambayo ilipata hitilafu kwenye eneo lenye kona
No comments:
Post a Comment