Friday, January 17, 2014

AADA YA MAINDA KUTANGAZA KUOKOKA NA KUMRUDIA MUNGU, HUYU NDO MSANII MWINGINE WA BONGO MOVIE ALIYETANGAZA KUOKOKA


Salome Ndumbagwe Mesayo ‘Thea’.
WASANII wa filamu, Ruth Suka ‘Mainda’ na Salome Ndumbagwe Mesayo ‘Thea’ sasa wameonekana kujikita zaidi kwenye mafunzo ya kiroho baada ya hivi karibuni kunaswa kwenye kongamano la ukombozi ndani ya Ukumbi wa Vatican City Sinza jijini Dar walipokwenda kuabudu.
Ruth Suka ‘Mainda’.
Wawili hao walinaswa wakiwa na nyuso za unyenyekevu huku wakionekana kudhamiria kumrudia Mungu na walipoulizwa walisema walikuwa katika kongamano hilo la mafunzo ya kiroho na Biblia kwa siku tatu.
 
 “Sisi tumempokea Yesu, tunawasihi wasanii wenzetu waachane na ushirikina waje huku ambako kuna njia salama, hili ni kongamano ambalo lina mafunzo mema na lina uwezo wa kumbadili mtu kutoka kwenye roho ya kishetani na kuwa na roho safi,” alisema Thea....
CREDIT : GPL

source bongo clan

No comments:

Post a Comment