Thursday, February 27, 2014

Universal secrets......!!

Habari zenu wapendwa,
kuna hiki kitu kinaitwa universal secrets, yaani siri za ulimwengu au siri za dunia hii tunayoiishi. Kawaida mtu unazaliwa na unaanza kupata kumbukumbu at least kuanzia miaka miwili na nusu au mitatu ila tangu ukiwa umezaliwa hadi kufika miaka mitatu hata umeditate vipi huwezi kukumbuka zaidi yake utahadithiwa kuwa ulikuwa mlizi sana, ulikuwa hupendi watu, ulikuwa unapenda kula, ulikuwa mjanja na uliwevuka haraka kuliko umri n.k

Kilichonifanya nifikirie kuhusu hizi universal secrets ni kuwa pale hasa kutoka miaka 0 hadi 3 kama watu wangekuwa wanazaliwa wanaongea wangetoa siri za universal maana ile lugha hakuna anayeweza kuijua na ndio maana watu husema watoto wachanga ni malaika.

Mfano mawasiliano ya mtoto na mama huwa ni ya kuguess kuwa mtoto huyu akilia anataka nini au kwa nini leo halali hana usingizi kabisaa au leo kalala sana. Iwapo watoto hawa wangeweza kusema wangetoa siri nyingi za dunia na ulimwengu huu.

Kilichonisukuma hasa kuandika uzi huu ni baada ya kusoma ule uzi wa kusoma saa kinyume na mshale unavoelekeza, hadi naingia mitamboni hakuna aliyekuja na jibu sahihi, wengine wakasema ni free masons and the like ila to me ni universal secrets. Na mwanadamu anapotafuta kujua universal secrets ndo hapo mtu anaenda beyond thinking yaani anakuwa yuko ulimwengu mwingine na anapokuja na data kujaribu kuzishare na dunia hakuna anayemuelewa na wengine wanamuona chizi.

Hii ni pamoja na wanaokuja na stori za kusema walishawahi kufa na kufufuka na muda wamekufa vitu walivyoona wakivisimulia huku duniani huwa wanadhihakiwa kuwa hawakufa bali walizimia na hivo wanavosimulia wanaambiwa ni ndoto tuu au maluweluwe yamewapanda kichwani na watakuwa wanasumbuliwa na malaria.

Sasa basi naomba wanajamvi wote wenye interest na hii universal secrets kuchangia chochote unachojua kuhusu siri za dunia hii japo wapo wanaosema ukifanikiwa kuzijua siri za ulimwengu huu huwezi kuishi utakufa tuu.

Ushawahi kusikia watu wakisema watoto wachanga huwa waanaona wachawi?
Kuna wanyama pia wanashirikishwa kwenye siri hizi za ulimwengu kama mbwa na paka, je unalolote zaidi ya haya ambayo ungependa kutushirikisha, karibu kuchangia.

Wednesday, February 26, 2014

Bunge La Katiba; Kila Mbunge Ana Dakika Moja Na Nusu Tu Ya Kuongea Katika Siku 90..!
Ndugu zangu,

Kwa Wabunge wetu wateule Bunge la Katiba kuendelea kupoteza muda kujadili posho na kanuni ambazo hazijakaa sawa mpaka sasa ni kuzidi kupoteza muda kwa kazi ambayo wananchi tulitarajia waende wakaifanye kule Dodoma; kujadili na kupitisha rasimu ya pili ya Katiba yenye kutokana na mawazo ya Wananchi.

Sijui kama kuna Wabunge wengi wateule wenye kujua, kuwa hata kama watakaa Dodoma kwa siku 90, bado, kwa hesabu za Kisayansi, hiyo ina maana ya dakika 54,000. Ukizigawa hizo kwa wajumbe 600 tu, unapata wastani wa dakika moja na nusu kwa siku ya kuongea kwa kila mjumbe. Ni kwa siku 90 na kwa kuchukulia kuwa watafanya kazi kwa saa kumi kwa siku, kuanzia Jumatatu mpaka Jumapili.

Hivyo, kwa hesabu hizo, nauona ukweli, kuwa hata hizo siku 90 hazitawatosha wajumbe wa Baraza la Katiba, endapo, sura ya hali itakavyokuwa Bungeni itakuwa kama inavyoonekana sasa. Hali ya mivutano na hasa kama Bunge hilo litaamua kufanya kazi ya kubadili vifungu vya rasimu hiyo na hata kuweka vipya.

Maana, kutahitajika mjadala mrefu. Na mjadala huo utatoka hata nje ya Bunge, kwa maana, wananchi nao watakuwa wakijadili kupitia vyombo vya habari na kuathiri upepo wa majadiliano ndani ya Bunge. Hivyo basi, kutakuwa na hali ya kuahirishwa vikao mara kwa mara na siku pia kuongezeka.

Nahofia pia, kuwa Wabunge wazoefu kwenye kuzungumza ndio watakaozungumza, na hivyo basi, watakuwa wamekula muda wa wenzao. Na matokeo yake, ni ukweli kuwa, kuna wabunge walioko Dodoma sasa, watakaozimaliza siku 90 kwa kuishia kupiga kura tu, na si kujadili Katiba wakasikika na kuonekana na waliowatuma kwenda Dodoma
Najaribu kufikiri sana: TUNAKUMISS SANA J. K. NYERERE
Najaribu kufikiri sanaaaaaa

TUNAKUMISS SANA J.K.NYERERE

1. Idd Amini - Alipoivamia Tz....Mwalimu alitamka tutampiga nduli!.. Na kweli Idd Amini alipigwa hadi akaikimbia Uganda.......

2. Kolimba - Alipotamka CCM imepoteza Dira na Mwelekeo...Mwalimu alimwita Dodoma akamuuliza nani kakutuma useme hivyo?!.. Ndio ukawa mwisho wa Kolimba!..

3. Samweli Sitta - Alipokuwa kiongozi wa serikali ya wanafunzi pale UDSM aliongoza mgomo wa wanafunzi wenzake kudai siagi na maziwa!... Mwalimu aliibuka pale chuoni akamuuliza Samweli "Samweli kwenu mnakunywa maziwa kweli?!.." Akamwambia lala chini, akamcharaza bakora na mgomo ukaishia hapo hapo!...

4. Abdul Jumbe! - Alipotaka serikali tatu!.. Nyerere alimuuliza moja kujumlisha moja ni ngapi?!.. Jumbe akajibu ni mbili!.. Nyerere
akamwambia kama ni mbili mbona unataka serikali tatu?!.. Huo ndio ukawa mwisho wa Abdul Jumbe kuwa Rais wa Zanzibar!..

5. John Samwel Malecela - Ni baada ya taarifa kuzagaa kuwa amebadili dini na jina ili apate kuungwa mkono na nchi za kiislamu kugombea Urais mwaka 1995!..Nyerere alimwambia wee John wewe umeenda Arabuni mara moja umebadilisha jina sasa unaitwa Jumanne!. Ukienda mara ya pili si utabadilisha kabila?!... Huo ukawa mwisho wa ndoto zake kuwa Rais wa Tz !...

6. Edward Lowassa-Alipokodi ndege binafsi ikampeleka hadi dodoma kwenye vikao vya mchujo wa wagombea Urais kupitia CCM mwaka 1995 alimpa lift JK!..Nyerere alimuuliza mmekuja na Ndege dodoma pesa mmetoa wapi?!.. Jina la Lowassa likakatwa kabla ya vikao vya mchujo!..

Wakamuuliza Nelson Mandela,tukupe nini ili uache usumbufu na harakati zako,wakampa cheki ajiandikie kiasi cha fedha,yeye akaigeuza kwa nyuma akaandika UHURU NA USAWA WA WATU WANGU-

Hakuna tena mfano wa viongozi hawa siku hizi.
Wataalamu wa sheria na mambo ya katiba serikalini walipotoa Hadidu za Rejea na kuikabidhi Tume ya Jaji Warioba kwa kupitia mkono wa Rais Kikwete, kuna wengine walidhani safari ya kisiasa kupata Katiba Bora waliyokuwa wanasafiri bila kufahamu walipo na wanakoenda, basi watakuwa wamefika.

Mwingereza anayejulikana kwa jina la kalamu kama Lewis Carroll alishawahi kusema, If you don’t know where you’re going, any road will get you there.

Well, kuna wanasiasa hawakufahamu kwa nini Hadidu za Rejea zilikuja na misingi kumi ambayo iliambatana na sheria ya mabadiliko ya Katiba 2013 iliyoacha milango ya kisheria wazi ambayo kwa sasa inatafsiliwa kwa namna yoyote bila hata kuvunja sheria. Wengine wanasema kazi ya Bunge la Katiba ni koboresha, huku wengine wakisema, kazi yake haina mipaka kisheria.

Majibu yake kwa sasa ndiyo haya yameanza kujitokeza kutoka kwa viongozi wakuu wandamizi wa serikali. Kama kuna viongozi wa siasa au vyama hawakufahamu kusuka au kunyoa lakini kwa sasa wako kwenye Bunge la Katiba, basi acha wanyolewe au wasukwe na serikali ya CCM ili wajitambue katika nafasi zao za kisiasa.

Waziri Mkuu ni mjumbe tu kwenye Bunge la Katiba pamoja na kwamba ni Mwenyekiti wa wabunge wa CCM lakini huwezi kuondoa msingi wa athari za matamko yake katika jamii. Kwa sasa yuko pale kutetea hoja na sera ya chama chake ambacho kina wanachama 'milioni tano'.

Hii ndiyo habari ya Mjini. Mnaotaka Serikali ya Tanganyika, mnakusudia Tanganyika ipi?. Tanganyika ya mkoloni au ya baada ya uhuru ya miaka mitatu!,

Mimi ninachotaka ni kuvunja Muungano au kama haiwezekani, basi serikali moja itanitosha kwa miaka 50 ijayo. Siitaki Tanganyika kwa sababu zijawahi kuiona. Sihitaji serikali mbili kwa sababu hazijajenga mazingira halisi ya serikali mbili. Serikali tatu ni kupoteza muda tu kwa sababu haziwezi kudumu. Serikali nne ni kuongeza gharama wakati shule hazina hata ubao wa kufundishia achilia mbali chaki na madawati.

Unapoona wingu linatanda, huna budi kutarajia mvua kunyesha lakini vile vile disappointment is all part and parcel of Homo sapiens.


Mizengo Pinda: Mnaitaka Tanganyika ipi?.
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amekiri kuwa Bunge Maalumu la Katiba, limeanza na changamoto, huku akihoji wanaotaka Serikali ya Tanganyika, wanakusudia ipi ya mkoloni au ya baada ya uhuru ya miaka mitatu.

Mbali na hilo, amesisitiza yeye na chama chake cha Mapinduzi wanataka mfumo wa serikali mbili na si tatu kama Rasimu ya Katiba ilivyopendekeza.

Amekiri kuwa uchaguzi wa Mwenyekiti wa Bunge unaotarajiwa kufanyika wiki ijayo, utakuwa na misukosuko mingi, lakini utavuka salama.

Pinda aliyasema hayo jana wakati akifungua semina ya viongozi na watendaji wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwenye Makao Makuu ya chama hicho, White House mjini hapa.

Pinda ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, alisema zipo hoja nyingi za msingi katika mchakato huo wa kutunga Katiba, lakini kubwa na litakalochukua muda mwingi ni muundo wa Serikali. Hata hivyo, alisema wazi msimamo wake na ule wa CCM kuhusu pendekezo lao la kuwa na Serikali mbili, kinyume cha Rasimu ya Katiba inayopendekeza Serikali tatu.

“Hata ukiniamsha usingizini usiku wa manane, kwangu mimi bado Serikali mbili ni muundo mahsusi.

“Mwalimu Nyerere hata wakati ule alikaa na Tanganyika kwa kipindi kifupi, mwaka 1961 Tanganyika ikawa huru, 1962 tukawa Jamhuri, 1963 Zanzibar ikapata uhuru (baadaye alisema Uhuru wa bandia), mwaka 1964 ikazaliwa Tanzania.

“Tanganyika ya kikoloni ndiyo iliyokaa muda mrefu, hii nyingine ni kutoka mwaka 1961, 1962 na 1963. Ikazaliwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Leo hii miaka 50 tuko ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tunadai Tanganyika,” alihoji Pinda na kuongeza:

“Tanganyika ipi? Nikadai ile ya mkoloni? Kipi kimo katika Tanganyika ya miaka mitatu? Tanganyika wakati inazaliwa nilikuwa na miaka 13, Tanzania nilikuwa na miaka 16, naujua vizuri Muungano. Kuanzia pale sijui chochote kingine, kama ilivyo wengi wetu humu.

“Au wale waliozaliwa miaka 50 iliyopita, wanaijua vizuri zaidi Tanzania. Tanganyika ipi mnazungumzia? Maana haikuwapo zaidi ya ile ya kikoloni iliyokaa muda mrefu.”

Alisema njia bora ni kukaa chini na kuzungumzia matatizo ya muundo wa Serikali mbili na kuyaboresha kwa nia ya kusonga mbele kuliko kudai Serikali ya Tanganyika. Waziri Mkuu alisema si vyema kuanza sasa kujaribu muundo wa Shirikisho baada ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, huku akitolea mfano wa Shirikisho la Afrika Mashariki (EAC).

“Pale kuna Shirikisho la Afrika Mashariki, lakini angalia mambo yanavyokwenda sasa wakubwa wakikutana. Utasikia wanazungumzia ardhi, mara pasipoti.

“Haiwezekani miaka 50 baada ya Muungano tuanze majaribio ya Shirikisho. Aah, wapi tunataka kwenda. Tanzania Bara na Zanzibar wana historia ya udugu na ushirikiano. Ukaribu, lugha moja na kuoleana,” alisema Pinda.

Huku akirejea kauli mbalimbali za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, alisema hata hilo Shirikisho linalopendekezwa litakwama, kwa sababu Rais wake hatakuwa na ardhi, na kama nchi wanachama zitakataa kutoa ardhi, atafanyaje kazi zake.

Alisema tatizo lililopo ni utambulisho wa Zanzibar na suala la umiliki wa ardhi kwa Tanzania Bara wakiwa visiwani, ambayo alisema ni mambo yanayozungumzika.

“Suala hapa ni utambulisho wa Zanzibar ambalo hata hivyo si suala kubwa na tunaweza kulisahihisha. Pia liko suala la ardhi Zanzibar. Lakini wanaotaka ardhi huko, lazima wajiulize je, kweli iko ardhi ya kutosha,” alieleza.

Akizungumzia Bunge Maalumu la Katiba alisema, “Tumeanza mchakato wa kutunga Katiba, lakini tayari kuna changamoto zetu, lakini tumeanza kwa kuchagua Mwenyekiti wa Muda na kutengeneza Kanuni wiki ijayo zitakuwa tayari ili tulifikishe mwisho hili,” alisema na kuongeza:

Bunge Maalumu la Katiba limeanza vikao vyake wiki iliyopita, lakini wiki ijayo linatarajiwa kuanza mijadala baada ya kupitishwa kwa Kanuni na kuchaguliwa kwa Mwenyekiti na hatimaye kuzinduliwa rasmi.

Hata hivyo, tayari kuanza hali ya sintofahamu kwa wabunge kuanzia kudai suala la nyongeza ya posho, hadi katika vikao vyao ya kazi ambako zimeshuhudiwa kauli zinazoashiria kazi nzito mbele na inayopaswa kuwa na udhibiti ili mijadala isitawaliwe na jazba na kutekwa na makundi yaliyowapeleka bungeni humo.

Aliwaomba wajumbe wa semina hiyo ya Jumuiya ya Wazazi kuwaombea wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, watimize majukumu yao kwa maslahi ya Taifa.

Tuesday, February 25, 2014

Wasomi na hatima ya tanzania
Ningependa kuuliza , hivi kweli Tanzania kuna wasomi? Na kama wapo je ni viashiria (indicators) gani vya kuonesha kuwa hii nchi ina wasomi tena wengi?

Naomba msinishangae kwakuwa aulizaye ataka kujua jamani, na kwakuwa nijuavyo mimi ni kwamba msomi ni yule anayetumia elimu yake kufanya vitu vinavyoonekana, haogopi kufukuzwa kazi kwa kutimiza wajibu wake kitaaluma, ni mkereketwa wa kweli wa nchi na rasirimali zake, hawezi kukwepa wajibu wake hasa pale wajibu huo unapoangukia kwenye eneo husika na alichosomea na ni muumini mzuri wa miiko ya taaluma yake.


Tanzania ya sasa ina professors wangapi? Ina PhD holder’s wangapi? Ms wangapi?
Muonekano wa kiuchumi, kisiasa na kijamii unahakisi idadi ya wasomi tulio nao nchini?
Tanzania ya enzi za wasomi wachache na ya sasa ni sawa?
Kama ni kinyume na muonekano bora, je tunaweza kujua ni kwanini tuna non performer scholastics nchini?

Nawasilisha wakuu.
Precision Air wamshusha Dr. Azaveli Rwaitama kwenye ndege kisa Lugha
Precision wamzalilisha Dr Azaveli Rwaitama mwanza baada ya kumutia polisi ndani ya ndege na kumshitaki kwa kosa la kukataa kutii amri za wahudumu. Kwa sasa anashikiliwa na polisi.

Alikuwa ameketi kwenye kiti cha emergence exit na kuwataka wahudumu wampe maelezo kwa Kiswahili kwani ndege za Precision ni za kitanzania na zinaoparate nchini. Wahudumu walikataa na kumwamuru ahame kama yeye hajui kingereza- Kwa kuanzia hapo polisi waliitwa na kumtia mbaroni.

Ninachojua mimi ni kwamba ndege nyingi hutumia Lugha kuu za kimataifa na Lugha za nchi husika. Ukipanda Ethiopia line au Turkish na zingine nyingi watakupa maelezo kwa Lugha yao ya Taifa na zingine za kimataifa. Inakuwaje leo Tanzania tushindwe kutoa flight instrusctions kwa kiswahili?

Precision mmemkosea Dr Rwaitama mwombeni radhi na mlipeni gharama zote za kusimamisha safari yake ya Bukoba.

-----------------------------------
Maelezo ya Dr. Azaveli Rwaitama

 By Alex Manonga View Post
Nawashukuru wote kwa kunipa pole. Wanasheria wa rafiki yangu binafsi Dr Antony Diallo, mmiliki wa Star Tv na Radio Free Africa, na wanasheria waliotumwa na Nd. Sungusia wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu ( Legal and Human Rights Centre, LHRC) chenye makao makuu Dar es Salaam walifika kituo cha polisi cha kiwanja cha ndege Mwanza na wakafanikiwa kuniwekea dhamana na hivyo niko nje kwa dhamana vinginevyo ningelala selo ndugu zangu _Kesho nitaripoti polisi kufuatilia juu ya kesi iliyofunguliwa dhidi yangu na Precision kanma itaenda mahakamani au vipi.

Kilichotokea kifupi ni hivi. Nilipanda ndege Flight PW 0492 iliyotarajiwa kuondoka Mwanza saa 3 dakika 50 asubuhi kuelekea Bukoba. Nilikuwa nimekaa kiti namba 2B na mtafiti mmoja anayefanya kazi Maruku Tea Estate huko Bukoba alikaa kiti na. 2A kwenye dirisha kushoto kwangu. Wakati ndege inaanza kukuelekea inakoruka alikuja mhudumu wa kike akatuuliza na yule mwenzangu kama tunajua Kiingereza na mimi nikasema kwa utani huku nikicheka kuwa tunajua kidogo. Yule muhudumu gafla akatahamaki akasema kama sijui kiingereza aniamishe kiti.

Mimi nikamjibu kuwa hakukuwa na haja maana mimi najua kiingereza maana ni mwalimu wa siku nyingi wa Kiingereza lakini nilichokuwa nashangaa ni kwa nini nyie wahudumu mnapenda kutoa maelezo kwa Kiingereza wakati mgeyatoa maelezo hayahayo kwa Kiswahili mara baada ya kujua kuwa sisi ni Watanzania na tunajua Kiswahili vizuri zaidi kuliko Kiingereza. Binti huyo nikaona ametaamaki na kuanza kusema lazima niteremshwe.

Mimi nilidhani masihala maana niliwahi kutoa ushauri huu hapo nyuma kwa mhudumu mwingine wa Precision Air na yeye alinijibu kwa heshima kabisa kuwa wao maelezo wameambaiwa lazima wayatoe kwa Kiingereza. Mara yule mhudumu wa kwanza akaondoka akaja mhudumu mwingine wa kike akasema kama sijui Kiingereza niamishwe nikamjibu wa taratibu na tabasamu langu la kawaida ninalolitoa katika mazingira kama haya ya dalili za kukosekana busara na mtoa huduma kukimbilia kwenye mambo ya kugombana bila sababu kuwa hakukuwa na tatizo jamani kwani Kiingereza nakijua na nilichokuwa nimempa mwenzake ni ushauri tu.

Yeye wala hata hakuzungumza na mimi tena aliondoka ndipo nikasikia rubani akitangaza eti kuna tatizo la kiusalama na ndege itachelewa kuruka ili litatuliwe. Mara polisi wane hivi na muhudumu wa Precision wa kiume mmoja wakaingia ndani ya ndege na kusimama mbele yangu nilipokuwa nimekaa na kufunga mkanda. Mhudumu akaniambia inabidi au nikuamishwe kiti au ni ushushwe. Wakati huo huo wale polisi wakang'angania eti lazima nishuke. Nikauliza nitii amri ya nanai sasa? Polisi mmoja aliyeonekana kama mwenye kuwaongoza wale polisi wenziwe akainama akanifungua mkanda wa kwenye ndge akaninyanyua mkuku mkuku na kunitoa nje ya ndege.Hata begi zangu mbili za mkononi ilibidi niombe nikiwa chini nipewe.

Abiria waliokuwa karibi na nilipokuwa walishangaa na kusema kwani amefanya nini huyu baba . Lakini waliokuwa nyumba mabali hawakujua kilichotokea zaidi ya manaeno waliokuwa wamelishwa na rubani na wlae wahudu kuwa kuna baba kule mbele amnaleta fujo inabidi ateremshwe. Nikapelekwa kituo cha polisi hapo uwajani huku nikisikia wakinongonezana kuwa lazima kuniweka selo (lockup ).

Nikafanikiwa kumpigia Dr Antony Dialo simu akazungumza nao wale askari na wakaanza kuchukua maelezo yangu nikiwa nimeketi ofisini kwao kwenye kochi walau badala ya kuwekwa lockup... Baadaye nilipigia Ndugu Sungusia wa LHRC na Dr Antony Diallo wote wakanitumia wanasheria walionisaidia kuandika na kutia saini maelezo yangu. Wale wanasheria wakaniombea dhamana nikapata nikaruhusiwa kutoka pale kituoni lakini nikaamriwa kuripoti kituoni pale asubuhi kesho Jumatatu kwa maelekezo zaidi.

Wakati huo ndege ile ya Precision iliondoka ikaenda Bukoba na ikarudi tena baadaye kutoka Bukoba na ndipo nikamuona yule muhudumu wa kike wa pili eti ndiye anatoa maelezo juu ya eti mimi kufanya fujo. Yule muhudumu aliyewadanganya wenzake wote pamoja na rubani kuwa eti mimi nimefanya fujo wala hakutoka nje ya ndege iliporudi kutoka Bukoba kutoa maelezo.

Katika sakata lote ili yule abiria aliyeketi kushoto kwangu siti namba 2A wala hakuhojiwa na rubani wa ndege ile kujiahakikishia kama madai ya eti mimi kufanya fujo yalikuwa ya kweli na wala hata polisi waliotekereza maelekezo ya rubani yakuniondoa ndani ya ndege mkuku mkuku hawakujiangaisha kuuliza yule abiria jirani yangu aliye kuwa siti 2A kama ni kweli mimi nilifanya fujo yoyote au nilitoa maoni tu juu ya matumizi ya Kiswahili katika kutoa maelezo ya juu ya kipi cha kufanywa wakati wa dharura.

Hadi sasa bado sijaelewa kisa kilichomfanya yule mhudumu atahamaki na kunibambikizia tuhuma ya kufanya fujo yarabi... maana hakukuwepo hata na kubadirishana maneno kwa ukali kwa upande wake au wangu. Nimebaki nimeduwaha hadi sasa kuwa hivi ni kweli miaka zaidi ya 50 baada ya uhuru nimekatishiwa safari yangu kwa kutoa maoni tu ambayo mhudumu yule wa shirika la ndege binafsi angeweza kupuuza.

Bado sipati maelezo kwa nini haya yalinitokea zaidi ya kuhisi kuwa haya ni matokeo ya mfumo wa kuandaa wahudumu wa ndege wa Precision unaowavimbisha kichwa kuwa kwa kutamka kwa rubani kuwa kuna abiria anafanya fujo hiyo inatosha abiria yule kunyanyaswa kama nilivyonyanyaswa na kudhalilishwa kwa kutuhumiwa kufanya fujo ndani ya ndege.

Lazima nikiri hata hivyo kuwa maafisa Kadhaa wa kituo cha polisi cha uwanja wa ndege pale Mwanza walinionesha uungwana sana na walikuwa wakarimu kwangu kuliko hata wahudumu wale wawili wa Precsion Air.iyeketi kushoto kwangu siti namba 2A wala hakuhojiwa na rubani wa ndege ile kujiahakikishia kama madai ya eti mimi kufanya fujo yalikuwa ya kweli na wala hata polisi waliotekereza maelekezo ya rubani yakuniondoa ndani ya ndege mkuku mkuku hawakujiangaisha kuuliza yule abiria jirani yangu aliye kuwa siti 2A kama ni kweli mimi nilifanya fujo yoyote au nilitoa maoni tu juu ya matumizi ya Kiswahili katika kutoa maelezo ya juu ya kipi cha kufanywa wakati wa dharura. ondoka ikaenda Bukoba na ikarudi tena baadaye kutoka Bukoba na ndipo nikamuona yule muhudumu wa kike wa pili eti ndiye anatoa maelezo juu ya eti mimi kufanya fujo.

Yule muhudumu aliyewadanganya wenzake wote pamoja na rubani kuwa eti mimi nimefanya fujo wala hakutoka nje ya ndege iliporudi kutoka Bukoba kutoa maelezo. o simu akazungumza nao wale askari na wakaanza kuchukua maelezo yangu nikiwa nimeketi ofisini kwao kwenye kochi walau badala ya kuwekwa lockup... Baadaye nilipigia Ndugu Sungusia wa LHRC na Dr Antony Diallo wote wakanitumia wanasheria walionisaidia kuandika na kutia saini maelezo yangu.

Wale wanasheria wakaniombea dhamana nikapata nikaruhusiwa kutoka pale kituoni lakini nikaamriwa kuripoti kituoni pale asubuhi kesho Jumatatu kwa maelekezo zaidi. walishangaa na kusema kwani amefanya nini huyu baba . Lakini waliokuwa nyumba mabali hawakujua kilichotokea zaidi ya manaeno waliokuwa wamelishwa na rubani na wlae wahudu kuwa kuna baba kule mbele amnaleta fujo inabidi ateremshwe. Nikapelekwa kituo cha polisi hapo uwajani huku nikisikia wakinongonezana kuwa lazima kuniweka selo (lockup ). tena aliondoka ndipo nikasikia rubani akitangaza eti kuna tatizo la kiusalama na ndege itachelewa kuruka ili litatuliwe.

Mara polisi wane hivi na muhudumu wa Precision wa kiume mmoja wakaingia ndani ya ndege na kusimama mbele yangu nilipokuwa nimekaa na kufunga mkanda. Mhudumu akaniambia inabidi au nikuamishwe kiti au ni ushushwe. Wakati huo huo wale polisi wakang'angania eti lazima nishuke. Nikauliza nitii amri ya nanai sasa? Polisi mmoja aliyeonekana kama mwenye kuwaongoza wale polisi wenziwe akainama akanifungua mkanda wa kwenye ndge akaninyanyua mkuku mkuku na kunitoa nje ya ndege.

Hata begi zangu mbili za mkononi ilibidi niombe nikiwa chini nipewe.hi kutoa ushauri huu hapo nyuma kwa mhudumu mwingine wa Precision Air na yeye alinijibu kwa heshima kabisa kuwa wao maelezo wameambaiwa lazima wayatoe kwa Kiingereza. Mara yule mhudumu wa kwanza akaondoka akaja mhudumu mwingine wa kike akasema kama sijui Kiingereza niamishwe nikamjibu wa taratibu na tabasamu langu la kawaida ninalolitoa katika mazingira kama haya ya dalili za kukosekana busara na mtoa huduma kukimbilia kwenye mambo ya kugombana bila sababu kuwa hakukuwa na tatizo jamani kwani Kiingereza nakijua na nilichokuwa nimempa mwenzake ni ushauri tu. na haja maana mimi najua kiingereza maana ni mwalimu wa siku nyingi wa Kiingereza lakini nilichokuwa nashangaa ni kwa nini nyie wahudumu mnapenda kutoa maelezo kwa Kiingereza wakati mgeyatoa maelezo hayahayo kwa Kiswahili mara baada ya kujua kuwa sisi ni Watanzania na tunajua Kiswahili vizuri zaidi kuliko Kiingereza.

Binti huyo nikaona ametaamaki na kuanza kusema lazima niteremshwe.ipanda ndege Flight PW 0492 iliyotarajiwa kuondoka Mwanza saa 3 dakika 50 asubuhi kuelekea Bukoba. Nilikuwa nimekaa kiti namba 2B na mtafiti mmoja anayefanya kazi Maruku Tea Estate huko Bukoba alikaa kiti na. 2A kwenye dirisha kushoto kwangu. Wakati ndege inaanza kukuelekea inakoruka alikuja mhudumu wa kike akatuuliza na yule mwenzangu kama tunajua Kiingereza na mimi nikasema kwa utani huku nikicheka kuwa tunajua kidogo.

Yule muhudumu gafla akatahamaki akasema kama sijui kiingereza aniamishe kiti. awashukuru wote kwa kunipa pole. Wanasheria wa rafiki yangu binafsi Dr Antony Diallo, mmiliki wa Star Tv na Radio Free Africa, na wanasheria waliotumwa na Nd. Sungusia wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu ( Legal and Human Rights Centre, LHRC) chenye makao makuu Dar es Salaam walifika kituo cha polisi cha kiwanja cha ndege Mwanza na wakafanikiwa kuniwekea dhamana na hivyo niko nje kwa dhamana vinginevyo ningelala selo ndugu zangu _Kesho nitaripoti polisi kufuatilia juu ya kesi iliyofunguliwa dhidi yangu na Precision kanma itaenda mahakamani au vipi.